Posted On : 2024-02-06
Mbunge wa Jimbo la Ilala Mhe. Mussa Azzan Zungu alishiriki kwenye siku maalum iliyoandaliwa na wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum. Siku hii imelenga kuwapa kipaumbele wanafunzi wote wenye mahitaji maalum kwa kuwakumbuka katika kutimiza mahitaji yao mbalimbali.
Mhe. Zungu aliupongeza uongozi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha kwa namna wanavyowajali wanafunzi hawa wenye mahitaji maalum, na kuangalia namna ya kuwawezesha vifaa mbalimbali ikiwemo Vitimwendo, Mafuta ya Ngozi, Fimbo za kuwaongoza wenye ulemavu wa macho nk. Mhe. Zungu aliahidi kutoa Tsh. Milioni 10 kutoka kwenye fedha za mfuko wa jimbo ili kuchangia zoezi la kununua vifaa mbalimbali vya wanafunzi wenye mahitaji maalum. Alimalizia kwa kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna anavyowapa kipaumbele watu wenye mahitaji maalum kwa kuwapa nafasi kwenye kada mbalimbali.
WAFANYAKAZI WA IFM WAADHIMISHA SIKUKUU YA MEI MOSI 2024
2024-05-01 |
CAPACITY BUILDING PROGRAMS FROM NAZIM HUSSAIN, A VISITING PROFESSOR FROM THE UNIVERSITY OF GRONINGEN, THE NETHERLANDS
2024-05-01 |
THE IFM ALUMNI MEETING AT IFM
2024-04-30 |
IFMSO WAKABIDHI MISAADA KWA MLEZI WA KITUO CHA KULELEA WATOTO YATIMA CHA AMANI, KILICHOPO ZINGA - BAGAMOYO
2024-04-17 |
PAYMENT PORTAL |
BROCHURES |
COLLABORATIONS |
HEET PROJECT |
IFM PROSPECTUS |
SHORT COURSES |
ALMANAC 2023/2024 |