Posted On : 2024-02-02
Umoja wa Wanafunzi waliosoma Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM Alumni) wamekabidhi vifaa vya TEHAMA, ikiwemo Projector tatu, kwa uongozi wa chuo hicho mnamo tarehe 19 Disemba 2023.
Zoezi hilo limeongozwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi ambaye pia ni Mwenyekiti wa umoja huo. Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo Dkt. Yonazi amesema, wamefikia hatua hiyo mara baada ya kuona umuhimu wa kuongeza vitendea kazi kwa uongozi wa chuo hicho ili kuongeza tija katika masuala ya taaluma.
Naye Mkuu wa Chuo cha IFM Prof. Josephat Lotto amemshukuru kwa namna walivyojitoa na kuona umuhimu wa kufanya hivyo. Prof Lotto ameelezea kuwa hatua hiyo imewapa furaha na faraja, na kupongeza kwa namna walivyojitolea huku akiahidi kutunza na kuvitumia vifaa hivyo kama ilivyokusudiwa.
WAFANYAKAZI WA IFM WAADHIMISHA SIKUKUU YA MEI MOSI 2024
2024-05-01 |
CAPACITY BUILDING PROGRAMS FROM NAZIM HUSSAIN, A VISITING PROFESSOR FROM THE UNIVERSITY OF GRONINGEN, THE NETHERLANDS
2024-05-01 |
THE IFM ALUMNI MEETING AT IFM
2024-04-30 |
IFMSO WAKABIDHI MISAADA KWA MLEZI WA KITUO CHA KULELEA WATOTO YATIMA CHA AMANI, KILICHOPO ZINGA - BAGAMOYO
2024-04-17 |
PAYMENT PORTAL |
BROCHURES |
COLLABORATIONS |
HEET PROJECT |
IFM PROSPECTUS |
SHORT COURSES |
ALMANAC 2023/2024 |