Latest News and Updates



Posted On : 2024-02-06


KUSAINIWA KWA HATI YA MAKUBALIANO KATI YA IFM NA MKOA WA PWANI KUPITIA MRADI WA HEET


CHUO CHA USIMAMIZI WA FEDHA KIMESAINI HATI YA MAKUBALIANO NA MKOA WA PWANI KUPITIA MRADI WA HEET – TAREHE 17 JANUARI 2024

Katika kutekeleza dhima yake ya kutoa elimu na mafunzo kwa kiwango cha juu, ili kuibua uvumbuzi na ubunifu utokanao na tafiti na ushauri elekezi, Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha, Prof. Josephat Lotto, na Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani, Bw Rashid Mchatta, wamesaini ya makubaliano inayohusisha IFM na Mkoa wa Pwani.

Makubaliano haya yatasaidia taasisi hizi mbili katika nyanja za utafiti unaolenga kutatua changamoto mbalimbali kwa wananchi, na kutoa elimu katika nyanja tofauti kwa wafanyakazi wa Mkoa wa Pwani. Utiaji saini ulishuhudiwa na wahusika wakuu, kwenye utekelezaji wa makubaliano, wa pande zote mbili.

 

PAYMENT PORTAL

PROGRAMME BROCHURE

COLLABORATIONS

HEET PROJECT

IFM PROSPECTUS

SHORT COURSES

ALMANAC 2023/2024





CONTACT US

Main Campus
contact our main campus via
P.O Box 3918, 5 Shaaban Robert Street
11101 Dar es salaam
+255 22 2112931-4
Fax : +255 22 2112935
rector@ifm.ac.tz